Kujifunza web design na ukaimaster vizuri ni rahisi sana ikiwa tu utapata mtu anayejua na amekuwa akifanya hiko kitu miaka mingi kuliko kukomaa mwenyewe.
Utapita njia fupi ambayo ulitakiwa kujifunza miaka mitatu wewe ukajifunza ndani ya mwezi mmoja au miwili. Hapo unapata muda mwingi wa kutafuta wateja, kufanya kazi za kampuni zinazohusu website.
Pia utaokoa fedha nyingi. Mimi kipindi najifunza web design huko YouTube na kwingine hasa mwaka 2023 pesa ya bundle kwa siku ilikuwa 3k kwa 6k na hapo huna client na unajibana ukipiga kwa mwezi ni 60k+
Vingine nimekuja kuvielewa 2024. Hapa katikati 2023- 2024 kuna pesa nyingi sana imepotea lakini kidogo ukipata wateja ndio mambo yanakaa mkao.
Maisha ya kujifunza mwenyewe ni stressful na pengine usijue mambo kwa kina ila ukipata mtu wa kukufundisha na ukawa serious ni simple sana. Haichukui muda.
Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting
Baadhi ya matatizo yanayotokea kwenye website kama loading time, performance, critical error na kushindwa kufanya baadhi ya changes hutokea kwa sababu ya hosting service uliyonunua.Wakati mwingine huwa ni teknolojia mbovu ya hosting (Outdated).Kabla ya kununua au...
0 Comments