Kuna swali niliwahi kuulizwa “Kama ninapata wateja na kila kitu ninachokitaka kupitia mitandao ya kijamii je, kuna umuhimu gani wa kuwa na website”
Vipi kama ungelikuwa na website, si ungekuwa unapata wateja mara mbili zaidi?
Okay, social media siyo majukwaa yako muda wowote algorithms inaweza kubadilika, akaunti yako inaweza kufungiwa muda wowote.
Mtandaoni unaweza ukawa unapost vitu ambavyo haviendani na career yako/ business yako lakini kuna mtu akawa interested kujua zaidi “Huyu mtu anafanya nini” kama haweza kupata majibu ya direct mpaka aanze kuscroll kwenye post zako huenda na wewe wiki nzima unapost unrelated stuff maana yake hawezi kujua who you’re, what you do. Utapoteza fursa.
Ni vigumu kuonyesha testmonials zote kwa pamoja, ni vigumu kuonyesha nini unafanya ama nini kampuni yako inafanya kwa kina ili kwamba mtu akiangalia aelewe deep nini anaweza kufaidika kutoka kwako kabla hata hajakupigia simu.
Pili, unakuwa limited kuandika post ndefu sababu ya platform yenyewe ilivyo watu wengi hawawezi kusoma maneno mengi kiasi hicho (mfumo wa usomaji post ndefu siyo rafiki).
Tatu, visibility yako kwa search engine ni hafifu. Watu wakisachi huduma au bidhaa kama yako huwezi kuonekana kwenye SERP (Search Engine Result Page).
Hata kama kuna post ulijieleze au ulielezea nini kampuni yako inafanya mtu hawezi kuscroll post zote hadi aipate hiyo post. Kwanza hiyo post hajui kama ipo.
Unataka kukusanya emails za watu ili uwe unawapatia updates kuhusu biashara yako. Social media haina tool hiyo.
Website inatatua matatizo yote hayo na mengine mengi ambayo zijayataja. Kwa hiyo kama unategemea social media pekee fikiria mara mbili huenda ukafaidika zaidi ukiwa na website.
Huenda kuna watu wanamaswali kuhusu wewe ila ukiwawekea testmonials pale na maelezo mengine huenda ukaongeza trust kwa watu wengi.
Hata wote unaowaona kwa social media wenye akaunti kubwa kubwa kwa social media ukiwaangalia profile zao lazima utakuta kuna link ya either website yake au kampuni yake.
Sidhani kama kuna mtu huko mtandaoni yuko serious na kazi yake lakini hana website.
0 Comments