Jinsi ya Kuuza Bidhaa, Ujuzi Kupitia WhatsApp Business

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a Web Designer and Hosting @Tanzlite | Content Writer

December 22, 2023

Siku moja nilikuwa nimekaa zangu ghetto mida ya saa kumi na mbili jioni nasoma Hekaya za Abunuwasi, ghafla ujumbe ukatumwa kupitia WhatsApp kutoka kwa rafiki yangu akisema nimsaidie kutangaza hard disc drive aliyokuwa anauza.

Bila hiana kesho yake nikaipost kwenye status yangu, wakati huo sina uhakika kama kuna mtu anaweza kuinunua lakini baada ya muda mfupi  habari njema zikaanza kuonekana kwenye whatsApp chat, maswali yakawa mengi wadau wanauliza bei na kupita hivi.

Bahati nzuri kuna jamaa mmoja kweli alikuwa anahitaji hard disc kwa sababu compyuta yake ilikuwa na space ndogo so akanifuata DM na hatimae aliinunua hiyo disc kutoka kwa jamaa yangu baada ya kumpa maelekezo.

Tangu siku hiyo, fikra zangu kuhusu WhatsApp zilibadilika kabisa nikajisemea moyoni “Kumbe WhatsApp inaweza kuwa iko vizuri zaidi kuliko Twitter na Instagram!” Kwamba kupitia status unaweza kuuza kitu chochote na watu wakanunua. 

Unapataje wateja?

Kama nilivyotangulia kusema hapo awali hata mimi nilikuwa sina imani saana kama hiyo Hard Disk inaweza kununuliwa ila kitu nilichojifunza ni kuwa mteja ni yeyote yule anayeweza kuona status zako. Mtu yeyote mwenye uwezo wa kuona status yako huyo ni mteja. Anaweza asiwe mteja wako wa moja kwa moja lakini akawa na marafiki zake wanaohitaji bidhaa unayouza.

Kuna uwezekano mkubwa wa kutokuuza ujuzi ulionao au kupata mteja papo hapo. Yaweza kuchukua wiki au miezi ndo unaanza kupata wateja hao. Siku moja nilikuwa napiga story na jamaa yangu anaitwa kastory wengi wanamfahamu kama Castroelectronics alisema “Huwezi amini mwanangu vitu vyangu vingi huwa nauza kupitia status”.

Haikugharimu chochote kupost vitu unavyouza kwenye WhatsApp status yako. Unajua vijana wengi tunaogopa kujulikana kuwa tunafanya biashara fulani ndo mana huwa hatupost chochote ni meme mwanzo mwisho. 

Ikiwa wewe ni mjasiriamali au ndo unaanza pata muda zaidi ujifunze jinsi ya kutumia WhatsApp business kuuza na kutangaza biashara yako.

Haya ni maisha yako unamwogopa nani, unahofia nini. Halafu ukumbuke kuishi kwa kuangalia watu wengine watasemaje, watakuonaje ni sawa na kujichimbia shimo la umauti. Ulizaliwa peke yako utakwenda peke yako. WhatsApp ni fursa moja nzuri ambayo wachache wanaojua kuitumia vizuri wanafaidika sana.  

WhatsApp Channel na WhatsApp Group.

Kabla ya kuongezwa kwa WhatsApp channel feature wengi walikuwa wanatumia whatsapp group kuendesha shughuli zao mbali mbali ikiwemo uelimishaji, seminas, kupashana habari pamoja na kufanya biashara zao huko. 

See also  Umuhimu Wa Kuwa Na Website Licha Ya Kutegemea Mitandao Ya Kijamii Kupata Wateja

Lakini kila kukicha mambo mapya yanaibuliwa leo hii tuna WhatsApp Channel inayokupa fursa ya kuwafikia mamilioni ya watu wanaokadiliwa kuwa ni 2.78billion na wanazidi kuongezeka kila siku. 

Wataalamu wanasema channel zote hupewa kipaumbele cha kuonekana kwa mtu yeyote anayetumia WhatsApp kwa sababu by default iko public, yeyote anaweza kufollow channel hiyo. Nadhani ulishawahi kuziona kwenye whatsapp yako kama ambavyo zinaonekana kwangu hapa. Vivyo hivyo hata channel utakayotengeneza itapewa upendeleo huo.

Jinsi ya kutengeneza WhatsApp Channel

Kutengeneza WhatsApp chanel siyo kazi ngumu, ni rahisi kabisa fanya kufungua application yako ya WhatsApp, nenda kwenye updates 

  • Angalia kuna alama ya kujumuisha ibonyeze.
  • Bonyeza Create channel.
  • Click continue 
  • Upload profile picture, Andika jina la channel pamoja na maelezo mafupi kuhusu hiyo channel yako yaani biashara yako inahusu nini (kwa ufupi).
  • Bonyeza Create Channel.

Hapo utakuwa tayari umeshatengeneza WhatsApp channel kinachofuata ni wewe kuendeleza channel yako.

Jinsi ya kutafuta fursa za kazi kupitia WhatsApp. 

Ikiwa bado unatafuta kazi au bado ni mwanafunzi, whatsapp ni sehemu nzuri ya kutangaza na kuonyesha uwezo ulionao juu ya kazi fulani. Rafiki yangu mmoja anasoma Arusha Tech niliwahi kumwambia “The best place for you to find jobs is WhatsApp“. Akasema “Anthony, unajua sijakuelewa vizuri“.

Ikabidi nimweleweshe. Leo hiii tunaongea mimi na wewe tuko hapa Arusha kesho na kesho kutwa huenda wewe ukapata kazi huko Itaba na katika hiyo kampuni akawa anahitajika website developer. Ukizingatia wewe ndo upo incharge ukitizama nani anaweza kufanya hiyo kazi huoni si utanipigia simu mimi ambaye ulikuwa unaona status zangu?

Je vipi kama ungekuwa unaona napost tu memes kila siku ungejua kama naweza kutengeneza website? Ungenipigia simu ili nichangamkie hiyo fursa? Naam naamini umenipata. No one knows tommorow.  

Fursa haziji ukiwa umelala. Nakumbuka pia siku za nyuma hapo nilikuwa nashiriki kwenye mijadala kwenye magroup ya watu wengine nilijitahidi kutoa mchango wangu kulingana na uelewa wangu kuhusu mada walizokuwa wanazungumzia na uhalisia wa mambo yalivyo, pale walipoenenda tofauti niliwaambia. 

Kwa sababu nilijua hii ni fursa ya kuwekeza jina langu miongoni mwa watu.

Aisee kama unajua unajua tu ilikuwa saa nne usiku kiongozi wa hilo group akanitumia ujumbe kama unavyosomeka hapo chini.

See also  Yajue Malengo 3 Kabla Ya Kutengeneza Website Yako

Mtu akianza kukutafuta kwa njia kama hivi ujue kuna kazi umefanya. Hizi ndiyo connection. Unatangaza na kukuza jina kwa style kama hii. 

Ninachotaka kusema ni kwamba fursa za kazi zinaweza kupatikana sehemu yoyote ile siyo lazima uende kuomba kazi maofisini hata kupitia whatsApp unaweza kufanikisha hili. Kuna kitabu kimoja nilikuwa nasoma kinaitwa “Mbele Ya Muda” kimeandikwa na Shukuru Amos, anasema kazi yake ya kwanza ilitokana na watu kuona makala zake ambazo pia alikuwa anazipost kwenye status yake.

Hao hao watu unaobonga nao, wanaoona staus zako kila siku wanaweza wakakurecommend sehemu kutokana na vitu ambavyo huwa unashare. 

Watu hatufanani leo hii mko wote sawa. Kesho mwenzako manager wewe mtafuta ajira kwa hiyo siku moja historia inaweza kukubeba manager kaona kuna kazi uwezekano wa kukujulisha au kukuita ni mkubwa kwa sababu alishawahi kuona mambo unayofanya.

Sasa vipi kama ungekuwa unaongea pointless tu ukiwa na wenzako. Je, unaweza kweli ukaitwa kwa style hiyo? Hapana huwezi. 

Chukulia hiyo ndiyo fursa ya kujitangaza na kuonyesha umahili wako huwezi kujua huko mbeleni mambo yanaweza kuwaje. Kuwa serious hiyo ni fursa itumie vizuri. 

Kupitia WhatsApp status.

Nimesema, vijana hasa wale wanaosoma huwa hawataki kuonyesha kile wanachokijua. Utakuta kwenye status ameweka memes mwanzo mwisho, picha zao mwanzo mwisho, vichekesho mwanzo mwisho yaani hakuna hata kiashiria kinachoonyesha ujuzi wao. 

Siyo mbaya lakini kitu cha kujiuliza ni kuwa unaacha nini kwenye vichwa vya waangaliaji wa status zako. Mtu akiangalia status zako mbili tatu kitu gani atabaki nacho kichwani kuhusu wewe?.

Kama kweli unataka kutafuta kazi kupitia WhatsApp jaribu angalau kuwa open kwenye status zako sema ni nini unajua, unafanyaje na unaweza kumsaidia nani.

Unaweza usione matokea kwa muda huo lakini baada ya muda utaanza kutafutwa. Hili nina uhakika nalo usimdharau mtu kwa kuangalia hadhi aliyonayo leo. 

Yote kwa yote mchukulie mtu anaeangalia status zako kama mwajiri wako wa baadae. Jiamini na career yako hata kama hutakuja kuwa huyo uliye leo naamini kuna kitu lazima utajifunza.  

Mwisho.

Suala la kusaka tonge mara nyingi huwa ni gumu lakini WhatsApp siku moja inaweza kubadilisha maisha yako. Maamuzi yako leo ndiyo matokeo ya kesho. Uwe na siku njema.

0 Comments

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You may also Like….

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Ukiamua kutumia digital platforms kutangaza huduma/biashara yako ili watu wengi waifahamu, wakutafute ufanye nao kazi (partners), wanunue bidhaa zako n.k inahitaji kujitoa muda wako, pesa na kuwa tayari kuendana na hali ya soko.  Kutumia majukwaa ya mtandaoni...

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Baadhi ya matatizo yanayotokea kwenye website kama loading time, performance, critical error na kushindwa kufanya baadhi ya changes hutokea kwa sababu ya hosting service uliyonunua.Wakati mwingine huwa ni teknolojia mbovu ya hosting (Outdated).Kabla ya kununua au...

You may also Like….

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Ukiamua kutumia digital platforms kutangaza huduma/biashara yako ili watu wengi waifahamu, wakutafute ufanye nao kazi (partners), wanunue bidhaa zako n.k inahitaji kujitoa muda wako, pesa na kuwa tayari kuendana na hali ya soko.  Kutumia majukwaa ya mtandaoni...

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Baadhi ya matatizo yanayotokea kwenye website kama loading time, performance, critical error na kushindwa kufanya baadhi ya changes hutokea kwa sababu ya hosting service uliyonunua.Wakati mwingine huwa ni teknolojia mbovu ya hosting (Outdated).Kabla ya kununua au...