Jinsi ya Kujiunga LinkedIn Premium Bure (na faida zake)

Written by Anthony Charles

Anthony Charles is a Web Designer and Hosting @Tanzlite | Content Writer

December 8, 2023

Je, ulishawahi kujaribu kujiunga linkedin premium ukashindwa? Ulishindwa kwa sababu ni ya kulipia? Linkedin premium ina faida gani? Au hujawahi kabisa kufikiria kuhusu Linkedin premium?

Hata mimi kipindi najiunga LinkedIn sikujua kama kuna Premium yake na sikujua kama naweza for free. Kuna siku Mentor wangu akanielekeza jinsi ya kuitumia na leo hii nimekusogezea hatua kwa hatua jinsi ya kujiunga Linkedin premium bure pamoja na faida zake.  

Kwanza ijulikane kuwa linkedin premium ni ya kulipia LAKINI inatolewa bure kwa mwezi mmoja tu wa mwanzo mara tu baada ya kujiunga.

Offer hii ni kwa yeyote ambaye ndio mara yake ya kwanza kujiunga Linkedin premium baada ya hapo atatakiwa kusitisha au kulipia ili kuendelea.  

Jinsi ya kujiunga Linkedin Premium Bure.

1. Nenda kwenye profile yako ya linkedIn.

Bonyeza profile yako, angalia chini sehemu iliyoandikwa “Try Premium for free, au Try Premium for TZS0”. Kwa yule ambae tayari ameshawahi kuitumia atakuta imeandikwa “Reactivate premium”. Bonyeza hiyo sehemu kama inavyoonekana hapa.

2. Jibu maswali utakayoulizwa.

Baada ya kubonyeza Try premium itakupeleka sehemu ambapo utatakiwa kujibu baadhi ya maswali kwa kutick vibox vilivyopo, bonyeza NEXT, waweza pia kubonyeza skip ili kuendelea 

3. Chagua huduma unayoitaka

Hapo kuna huduma nne ambazo LinkedIn huzitoa utachagua mwenyewe unataka ipi kati ya Career, Business, Sales Navigation Core au Recruiter

Kati ya huduma hapo juu bonyeza huduma moja unayotaka kufaidika nayo. 👇

4. Bonyeza Try 1 month free ili kuendelea.

5. Chagua njia ya malipo na jaza taarifa za malipo.

Hapa unaweza kutumia Mpesa visa card au kadi yako ya Bank kujaza taarifa zinazohitajika. Ikiwa huna visa kadi unaweza kutengeneza mpesa visa card  kwenye simu yako ndani ya dakika moja. 

See also  Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Kumbuka: hakuna pesa yoyote utatozwa ndani ya mwezi mmoja baada ya kujisajili ni BURE, hautakatwa pesa yoyote iliyopo kwenye kadi yako mpaka mwezi mmoja utakapoisha. 

6. Bonyeza Start my Free Trial.

Hapo utakuwa tayari umemaliza kujiunga LinkedIn premium bure ndani ya mwezi mmoja wa mwanzo.

LinkedIn hutoa offer hii kila baada ya mwaka mmoja maana yake ukijiunga leo kupata tena offer hii ni mwakani tarehe kama ya leo. 

Faida za kutumia LinkedIn premium.

1.  Fursa ya kusoma kozi mbali mbali bure. 

Kozi yoyote unayotaka kusoma mfano  Marketing, Recruiting processes, Graphic designing, SEO, Video Editing, Copyrighting, Human development n.k utazipata kwa 0TZS ni wewe na bando lako tu. 

Baada ya kumaliza kozi utatunukiwa cheti cha kumaliza kozi hiyo ambayo unaweza kuweka kwenye profile yako, sehemu ya Licence and certification kwa sababu watakupa Url ya kuweka pale. 

2. Fursa ya kuona nani ameangalia profile yako. 

Mara nyingi kama huna premium huwezi kuona ni kina nani wameangalia profile yako, kwa wale ambao hawana premium ukiangalia  who’s viewed your profile haionyeshi sura za walioangalia profile yako. Kwa hiyo premium itakupa fursa hiyo ya kuona watu wanaopekua ukurasa wako.

Fursa hiyo itakupa njia nzuri ya wewe kuangalia ni vitu gani ufanye ili uwavutie zaidi hao wanaopakua kurasa yako kwa sababu mtu hawezi kuangalia profile yako pasipo sababu yoyote.   

3. Fursa ya kutuma ujumbe kwa mtu yeyote Linkedin.

Baada ya kujisajili, utapata fursa ya kumtumia mtu yeyote ujumbe iwe ni 1st au 2st connection wako. Mfano, unataka kutuma ujumbe (Dm) kwa mtu uliyevutiwa na post zake lakini baada ya kubonyeza ile button ya Message unaambiwa “Message X with premium” au  kwenye ile message kuna kikufuli yaani huwezi kutuma ujumbe kwa mtu mpaka ujisajili na premium. 

See also  Kujifunza Web Design Ni Rahisi

Kwa hiyo ukishajiunga premium utapewa hiyo ruksa ya kutuma ujumbe kwa yeyote yule.

4. Fursa ya kutuma Inmail kwa waajili Linkedin. 

Kama utachagua career premium plan utapewa ruksa ya kutuma inmail kwa waajili utakaopendezwa nao ambao kwa namna moja ama nyingine wanaweza kuwa mkombozi wako kwenye suala la ajira/kazi. 

Kuna fursa nyingi pia kwa wale waajili wanaotafuta kuajili wafanyakazi kwenye kampuni, biashara zao kupitia LinkedIn. 

5. Inatoa taarifa kuhusu nafasi za kazi zinazotangazwa na makampuni.

Unaweza pia kusoma zaidi faida mbalimbali za Kutumia Mtandao Wa LinkedIn Mbali na Kutafuta Kazi.

Hivyo ndivyo unaweza kujiunga  linkedin premium bure kabisa. kama bado hujajiunga Linkedin unaweza kuangalia hapa jinsi ya kujiunga linkedin na jinsi ya kutengeneza profile itakayokupatia fursa.

Msisitizo; Usisahau kusitisha offer hii kabla siku 30 hazijapata kupita kwa msaada zaidi LinkedIn watakutaarifu kusitisha kwa kukutumia ujumbe kwenye email yako. 

3 Comments

  1. Mashalah III

    Well done 👍👍👍

    Reply
  2. Anton’s Mathewa Mwasenga

    Hii imekaa vyema sana bei siyo kubwa sana ukilinganisha na unachokipata.

    Reply
    • Anthony Charles

      Yeah, napenda wanavyofundisha pia course zao ziko updated kuendana na soko la sasa kuna madini mengi huko.

      Reply

Submit a Comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You may also Like….

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Ukiamua kutumia digital platforms kutangaza huduma/biashara yako ili watu wengi waifahamu, wakutafute ufanye nao kazi (partners), wanunue bidhaa zako n.k inahitaji kujitoa muda wako, pesa na kuwa tayari kuendana na hali ya soko.  Kutumia majukwaa ya mtandaoni...

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Baadhi ya matatizo yanayotokea kwenye website kama loading time, performance, critical error na kushindwa kufanya baadhi ya changes hutokea kwa sababu ya hosting service uliyonunua.Wakati mwingine huwa ni teknolojia mbovu ya hosting (Outdated).Kabla ya kununua au...

You may also Like….

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Jinsi Majukwaa ya Kidigitali Yatakavyokusaidia Kukuza Biashara Yako

Ukiamua kutumia digital platforms kutangaza huduma/biashara yako ili watu wengi waifahamu, wakutafute ufanye nao kazi (partners), wanunue bidhaa zako n.k inahitaji kujitoa muda wako, pesa na kuwa tayari kuendana na hali ya soko.  Kutumia majukwaa ya mtandaoni...

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Mambo Ya Kuzingatia Unapotaka Kununua Hosting

Baadhi ya matatizo yanayotokea kwenye website kama loading time, performance, critical error na kushindwa kufanya baadhi ya changes hutokea kwa sababu ya hosting service uliyonunua.Wakati mwingine huwa ni teknolojia mbovu ya hosting (Outdated).Kabla ya kununua au...