Harakati Za Mjasiriamali Kujikomboa Zinakumbwa Na Changamoto Nyingi

Harakati Za Mjasiriamali Kujikomboa Zinakumbwa Na Changamoto Nyingi

Elimu yetu ningeiona ya maana sana ingekuwa inafundisha kujitegemea. Leo hii tungekuwa na viwanda vingi. Tungekuwa na ajira nyingi wahitimu, wanazengo wangejipambania wao wenyewe.

Kidogo vyuo vya ufundi (VETA) wako vizuri. 👏

Saivi elimu inaandaa vijana wazee watakaoingia ofisini kutunga sheria za tunakula vipi, kuandaa vikwazo vingi ili wajasiriamali wasiweze kuendeleza biashara zao. Inaandaa vijana wazee ili waje kuwa wakusanya kodi hodari mtaani si kuwaza ni kivipi itawasaidia wajasiriamali.

Kabla hatujapata uhuru wakoloni walichukua vijana wachache wawasomeshe ili waje wawasaidie kukusanya kodi yaani mtu akifanya kazi kwenye kiwanda chao wanamlipa mshahara kidogo bado mshahara huo huo aje alipe matiti tax, head tax, family tax hapo bado mahitaji ya familia kuna michango ya hapa na pale.

Elimu yetu bado iko huko na serikali vile vile. Hata wale wanaongia ofisini hawaelewi the hustle na namna ya kuwasaidia wajasiriamali hawa, wanaohitaji leseni, vibari ili kuendeleza mapambano yao.

Wengine wanaelewa lakini mikopo inawakaba koo.

Tuachane na hayo. Mchakato wa kupata huduma serikalini siyo rafiki kabisa, utahudhuria ofisini kwao mpaka basi mara njoo na hiki njoo na kile, lipia hiki lipia kile, mbona mtu fulani hajasaini rudi, subiri wiki mbili mtu wa.. aaprove, nenda ofisi za TANU.

Nimehangaika sana na hawa watu I know. Kwenye kutaka pesa wako chap ila kumpa huduma mapema msitahiki aah!

Kila siku upo road utafikiri mimi ni mfanyakazi wa serikali. Vitu vingine havina umuhimu lakini utasikia hatuwezi kukuhudumia bila hicho kitu.

Harakati za mjasiriamali kujikomboa zinakumbwa na changamoto nyingi hasa kwenye nchi ambayo haitambui nguvu ya mjasiriamali kwa taifa.

Jifunze jinsi ya kutengeneza websites za makampuni, NGO, portfolio n.k

Jifunze jinsi ya kutengeneza websites za makampuni, NGO, portfolio n.k

Kujifunza web design na ukaimaster vizuri ni rahisi sana ikiwa tu utapata mtu anayejua na amekuwa akifanya hiko kitu miaka mingi kuliko kukomaa mwenyewe.

Utapita njia fupi ambayo ulitakiwa kujifunza miaka mitatu wewe ukajifunza ndani ya mwezi mmoja au miwili. Hapo unapata muda mwingi wa kutafuta wateja, kufanya kazi za kampuni zinazohusu website.

Pia utaokoa fedha nyingi. Mimi kipindi najifunza web design huko YouTube na kwingine hasa mwaka 2023 pesa ya bundle kwa siku ilikuwa 3k kwa 6k na hapo huna client na unajibana ukipiga kwa mwezi ni 60k+

Vingine nimekuja kuvielewa 2024. Hapa katikati 2023- 2024 kuna pesa nyingi sana imepotea lakini kidogo ukipata wateja ndio mambo yanakaa mkao.

Maisha ya kujifunza mwenyewe ni stressful na pengine usijue mambo kwa kina ila ukipata mtu wa kukufundisha na ukawa serious ni simple sana. Haichukui muda.

Introducing Tanzlite Host: The New Web Hosting Player in Tanzania

Introducing Tanzlite Host: The New Web Hosting Player in Tanzania

Earlier this year, we introduced Tanzlite Host. This is not just another name in Tanzania’s web hosting services; we’re rewriting the rules.

Here’s how our unique approach to business is setting us apart and why it’s the most profitable model in the industry:

A Different Kind of Web Hosting Business

At Tanzlite Host, we’ve flipped the traditional model on its head:

  • Web Design First, Hosting Second: We’re fundamentally a web design agency that provides hosting. This means every website we host, we’ve likely designed. This approach ensures that we’re not just hosting your site; we’re invested in its success from conception.
  • Volume vs. Value: While many competitors chase volume, we focus on value. One corporate website project with us can be equivalent to years of hosting renewals. For instance, our corporate website packages start at Tsh 670,000, which matches the cost of our ESSENTIAL hosting package for 7 years. This model reduces the churn associated with constant sales efforts.

Why Our Approach is More Profitable:

  • Long-term Relationships: In Tanzania, where SMEs might not last long, our model ensures that even if a client doesn’t renew, they’ve already invested significantly in design and development. This reduces the pressure of constant new sales to maintain revenue.
  • Service Over Sales: Our business thrives on retainer services, one-time revamps, and additional features. This creates a more stable income stream than the volatile sales cycle of domain and hosting packages.
  • Exclusive Design-Hosting Bundle: We rarely allow clients to purchase just hosting from us if they’ve had their website designed elsewhere. This exclusivity ensures that our hosting service is tied to our design expertise, creating a symbiotic relationship where both services enhance each other’s value.

The Best Offer in Tanzania:

Understanding the financial challenges of starting a digital presence, Tanzlite Host offers an unbeatable deal:

  • Free Hosting and Domain for One Year: If you choose us to design your website, you get your hosting and domain for free for the first year. No other provider in Tanzania matches this offer. It’s our way of empowering you to start your digital journey without financial barriers.

Conclusion:

Tanzlite Host isn’t just about hosting; we’re about partnership, design, and empowerment. Our approach, focusing on design first and hosting second, not only aligns with the needs of Tanzanian businesses but also positions us as the most profitable model in the industry. Karibu!

Yajue Malengo 3 Kabla Ya Kutengeneza Website Yako

Yajue Malengo 3 Kabla Ya Kutengeneza Website Yako

Malengo ya kuanzisha tovuti huwa yanatofautiana kulingana na mmiliki wa tovuti hiyo. Malengo yangu na yako yanaweza yakatofautiana kulingana na mitazamo, mahitaji yetu kuwa tofauti

Kimsingi watu wengi wanaoanzisha tovuti huwa na malengo ya kupata pesa. Ukizingatia mabadiliko ya sayansi na technolojia yalivyosaidia kuunganisha watu kuwa kama kijiji, imekuwa rahisi kwa wachache kufedha hizo.

Pale watu walipo ndio pesa ilipo. Kama watu wapo mtandaoni basi pesa zipo mtandaoni.

Tuangalie malengo makuu unayotakiwa kuyangalia kabla ya kuanzisha website yako.

1) Kuuza Bidhaa

Tovuti inasaidia kuuza bidhaa uliyonayo yaweza kuwa ni nguo, vitabu, vifaa vya kielectronic, accessories n.k Hii ndio njia kuu na rahisi wanayoitumia wajasiriamali wengi wa kidigitali. 

Wajasirimali wanatumia tovuti kwa ajili ya kuuza bidhaa zao za kimwili au kidigitali. Tovuti inawasaidia kufikia watu kutoka sehemu mbalimbali. Uzuri wake ni kwamba watu wanaweza kununua bidhaa yako kwenye tovuti na kila kitu kikamalizika bila kuonana na mteja.

Kama inavyowasaidia wengine hapa Tanzania hata wewe itakusaidia kutengeneza duka lako mtandaoni na kuuza bidhaa zako. Kuna baadhi ya watanzania wamehamishia maduka yao kwenye website baada ya kuona haiwagharimu sana.

Yeye anahakikisha tu anabundle, ana simu janja basi, kazi iliyobaki ni kuhakikisha atakayenunua bidhaa anafikishiwa bidhaa yake kwa wakati. Ukiwekeza kwa namna hii utashuhudia ukipigiwa simu na wateja ambao huwajawahi kuwafikiria hata siku moja.

Mteja wako anakachokuwa anafanya ni ku-click click tu bidhaa hii hapa. Ikumbukwe: watu hununua bidhaa kutoka kwa watu wanaowajua.

Wewe unataka uanze biashara yako ya kuuza bidhaa kwa njia ya website. Jiulize, watu wanakufahamu? Watu wanaifahamu hiyo website yako, Unafahamika huko mtandaoni? Brand yako ikoje?

Lengo hili huwa ni gumu sana kulifanikisha kama hutotia nguvu na juhudi katika kutangaza bidhaa au huduma unayotamani kuiuza huko kwenye majukwaa mengine ya kidigitali.

Website itakusaidia kufanya mauzo ya bidhaa yako lakini haina uwezo mkubwa wa kuleta watu kwenye hiyo website ukiondoa injini ya utafuta (Search engine). Wewe ndiyo mwenye jukumu la kuleta watu kwenye website hiyo.

Uwezo wako wa kushawishi watu waje kwenye website yako ndio utakaokupa uwezekano wa bidhaa yako kununuliwa. Siyo rahisi lakini inawezekana ukiamua.

2. Tovuti za Washirika (Affiliate websites).

Tovuti hizi huwekwa matangazo ya bidhaa au ya huduma inayotolewa sehemu nyingine. Ulishawahi kutembelea tovuti fulani halafu ukakutana na tangazo linakutaka ubonyeze kisha linakupeleka sehemu nyingine kwenda kununua bidhaa au huduma fulani?

Naam, hizo ndio affiliate websites ninazozizungumzia. Mara nyingi matangazo haya huwekwa kwenye blogs. Mtu anapokuwa anasoma makala fulani ndani yake kuna kuwa na matangazo yanayoonyesha biashara ya mtu mwingine.

Mtu akibonyenza tangazo hilo linampeleka kwenye website inayohusu tangazo hilo. Huko ndo anaweza kufanya kile watengeneza tangazo wamekusudia. Tovuti hizi huwasaidia wenye tovuti kulipwa na kampuni ambalo wamekubali waweke tangazo lao kwenye website zao.

Ikiwa na wewe unataka utengeneza website ya aina hii hauna budi kupata kuwa mwandishi wa makala au kurasa ambazo zitakuwa zinapata watembeleaji wa kutosha.

Kuna njia kadhaa ambazo unaweza kulipwa ikiwa umetengeneza tovuti yako na inapata watembeleaji wa kutosha 1. Paid per click: Mtu akibonyeza hiyo link (Tangazo) kuna asilimia mmiliki wa tovuti atakulipa. 2. Paid per contract: Mmiliki tovuti (wewe) unaingia mkataba na kampuni inayotaka iweka tangazo lake kwenye website yako.

Kwenye affiliate websites mara nyingi huwa haina faida sana kama huna watembeleza wa kutosha wa tovuti yako. Jinsi unavyokuwa na watembeleaji wengi ndivyo utakavyoongeza nafasi ya kulipwa zaidi kulingana na makubaliano kati yako na mwenye tangazo.

Kama ulishawahi kutembelea tovuti halafu ukakuta kuna matangazo ya BETPAWA sijui BET SASA enhee! Hiyo pia ni aina ya affiliate websites.

3) Kuuza Huduma

Hapa ndipo tovuti hutumika kuongeza ufahamu zaidi juu ya kile mtu au kampuni inakiuza. Naomba tuelewane maana unaweza ukachanganya kati ya huduma na bidhaa.

Huduma inaweza kuwa utengenezaji wa wavuti, hosting services, huduma za ushauri, utoaji wa elimu kuhusu kitu fulani.  Mfano: Mimi natoa huduma ya kutengeneza website na kuhost tovuti za watu wengine. Hii siyo bidhaa ni huduma. Mwingine anaweza kusema Graphic designing na mwingine akasema Coaching.

Kwa hiyo tovuti hizi ni kwa ajili ya kuuza huduma uliyonayo. Ukienda thecitizen (Mwananchi) wanatoa huduma ya habari (magazeti), kwa mtu ambaye anataka kuwa anapata taarifa zote basi atalipia kwa mwezi au kwa mwaka ili apewe ruhusu ya kuona kila Habari inayochapishwa.

Unaweza kuamua hata wewe tuseme unatoa elimu kuhusu bima, umuhimu wake, hasara n.k kwa njia ya kozi na ukaifunga kwenye tovuti ili mtu anapotaka kozi hiyo basi aweze kuilipia. Huku ndiko kuuza huduma ninakokumaanisha.

Kwa kumalizia kasome zaidi pia umuhimu kwa kutengeneza website katika nyakati hizi za kidigitali.

Umuhimu wa Kutengeneza Website/Tovuti 2024

Umuhimu wa Kutengeneza Website/Tovuti 2024

Mtu akikuangalia akaona huna website anaanza kukulianganisha na scams. Sababu biashara nyingi zilizo serious lazima utakuta zina website. Website inayobeba heshima ya biashara zao.

Website inampa mmiliki uwezo wa kufanya kile anachotaka ili kusudi ionekane yakipekee kwenye soko la kidigitali yaani akitaka website iwe na hiki, ifanye hiki, mambo gani aweke kwa namna gani, ni yeye tu.

Leo hii Akaunti zako za mitandao ikifungwa utabaki na nini au biashara yako ndio itakuwa imeshia hapo! Tafakari kisha chukua hatua.

Website ina faida kedekede kama ambavyo nimekuainishia hapa chini.

Uaminifu

Watu siku hizi hawaamini maneno kirahisi rahisi, hawaamini tu kile mtu anapost mtandaoni kwani kumekuwa na watu wengi sana huko mtandaoni wanaosema wanatoa huduma kama yako lakini ukiangalia hawana tovuti/website.

Wengi wanaamini biashara yoyote lazima iliyo serious ina website, wakikusearch halafu wakakukosa wanaanza kukutilia mashaka.

Ni mara ngapi umekuwa ukisikia au ulishawahi kuulizwa, “Je, una tovuti ninayoweza kuangalia zaidi huduma yako?” Siyo kwamba watu hawataki kununua bidhaa au kupata huduma yako! Hapana.

Wanataka kupata ushahidi na maelezo zaidi kwamba ni kweli unaweza kutimiza ahadi zako unazoahidi huko mtandaoni. Isije ukawaingiza chaka.

Ujue kila mtu anaweza kutengeneza akaunti Twitter (X), LinkedIn au Instangram lakini ni wachache wanaoweza kutengeneza website. Kuwa na website ni ishara ya kuwa wewe ni mwaminifu ndiyo maana watu huuliza una website?

Kuwa na website ni zaidi ya kuwepo mtandaoni—ni pamoja na kukujengea uaminifu wako katika enzi hizi za kidijitali. Inakuonyesha kwa wateja wako kuwa upo serios na biashara, kweli umewekeza katika biashara yako.

Bila website watu watakuwa wanakuangalia tu huko mtandaoni, utakuwa unapoteza fursa nyingi zinaenda kwa washindani wako ambao tayari wana website kali.

Tovuti/website hailali wala haichukui likizo. Ipo hewani masaa 24 ikikutangazia biashara yako. Ikiwa website imetengeneza kitaalamu, yenye mvuto, yenye maneno ya ushawishi ndani yake inaweza kukupatia faida mara dufu ndani ya muda mchache.

Website ni kwa ajili ya kuuza/kutangaza huduma yako

Shida ya makampuni mengi yanatengeneza website ili yaonekane yana website. Je hilo ndilo lengo! Website ni kwaajili ya kutangaza, kukuza biashara kisha ikupatie wateja watakaokulipa ili uwapatie huduma yako.

Usiruhusu website yako ikae tu kama haipo. Tengeneza tovuti itakayokupatia faida itakayoonyesha kazi zako, itakayotoa ushuhuda (wateja uliowahi kuwasaidia).

Imarisha uaminifu wako mtandaoni na sifa zako leo kwa njia ya website.

Tengeneza tovuti inayothibitisha unaweza kufanya unachosema, na uone jinsi inavyogeuka kuwa chombo chako cha thamani zaidi cha masoko mtandaoni.

Changamoto nyingine ambayo watu huwa wanakuja kulaumu kuwa website haisaidii. Unatengeneza website halafu huipromote yaani huitangazi kwenye mitandao ya kijamii muda huo huo unataka watu wengi waitembelee na upate wateja wengi kweli!

Website ndiyo makao makuu ya marketing ukitengeneza website isemee kwenye mitandao hivyo ndivyo unavyojitangaza na kuvutia wateja.  

Mtu atayetengeneza website atafanya upate wake ionekane kwenye search engine pale mtu anaposearch kitu mtandao basi website yako ipate kupendekezwa ionekana. Pia na wewe ufanye upande wako.

Website ni utambulisho wako mkubwa mtandaoni

Website itawafanya hata watu ambao walikuwa hawakujui wakujue kwa undani kwa muda mchache. Kuliko ile mtu aanze kuscroll kwenye social media akaunti zako halafu ndo akute huo mda ulikuwa unapost mambo unayoyajua mwenyewe unafikiri.

Ataendelea kukufuatilia? Kwenye mitandao ya kijamii unaweza kupost chochote ili uchangamane na watu wengine lakini kwenye website content zinazokaa pale ni zile za muhimu tu.

Yaani ni rahisi mtu kukupa umakini zaidi hata kumfanya akupigie simu kwa majadiliano zaidi.

Jarida la leo nchini marekani –Top website statistics you should know in 2024  linasema takribani website mpya 252,000 zimekuwa zikitengenezwa kila iitwapo leo ambayo ni sawa na kusema website 10,500 zinatengenezwa kila lisaa au website 3 kila sekunde.

Hii ina maanisha ni kwa jinsi gani website zimekuwa zikifaidisha wafanya biashara wengi. Hasa wafanya biashara wanaotamani kupanua na kutangaza biashara zao mtandaoni.

Ukitaka kutengeneza website kali itakayokutangaza vizuri kwenye digitali hakikisha unaangalia na kampuni, agency, developer au designer anayeelewa fikra za wateja wako nikimaanisha saikolojia ya website development.